Breaking News

Mpalestina awapiga risasi na kuwaua Waisrael 3


Scene of attack at Har Adar (26/09/17)
Watu watatu raia wa Israel wameuawa kwa kupigwa risasi na raia wa Palestimna katika mlango wa kuingia kwenye makao ya walowezi wa kiyahudi eneo la Har Adara lililo ukingo wa magharibi.
Mtu mwenye bunduki wa umri wa miaka 37 kutoka kijiji kilicho karibu pia alipigwa risasi na kufariki baadaye.
Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alisema mauaji hayo yamesababishwa na uchochezi upande wa palestina.
Mauaji hayo yanafanyika wakati mjumbe wa Rais Donald Trump eneo la Mashariki ya Kati Jason Greenblat, anapowasili Jerusalem kufufua mazungumzo kati ya Israeli na 
Map of area of attack
Ikulu ya Marekani inasema kuwa imejaribu kufanya mikakati wa kuyafufua mazungumzo tangu Donald Trump aingie madarakani mwezi Januari lakini hakujakuwa na dalili za kuwepo hatua.
Mazungumzo ya amani kati ya pade hizo mbili yalivunjika mwezi Aprili mwaka 2014.
Polisi wanasema kuwa mtu huyo mwenye silaha anayetajwa na vyombo vya habari nchini Israeli kama Nimer Jamal, alishambulia baada ya kugundua kuwa alishukiwa na walinzi karibu na mlango wa eneo la Har Adar.

Aliwapiga risasi walinzi wawili na polisi wa mpaka kwa karibu, na kumjeruhi vibaya mtu mwingine kabla ya kupigwa risasi na vikosi vya usalama.

Scene of attack at Har Adar (26/09/17)
Alitoka kijiji cha Beit Surik, karibu maili moja mashariki mwa Har Adar.
Eneo hilo liko karibu kilomita 18 kaskazini magharibi mwa Jurusalem.
Karibu Wapalestina 36,000 wana vibali vya kufanya kazi katika makao ya wayahudi ambapo ulinzi wa kuyalinda dhdi ya mashambulizi ni mkali.
Zaidi ya wayahudi 600,000 wanaishi karibu makao 140 yaliyojengwa tangu mwaka 1967, kwenye ukingo wa magharibi na Mashariki mwa Jerusalem.

A photo of the gun used by the attacker, released by Israeli police


x

No comments