Breaking News

Barnaba Aajiri Bodigadi, Aeleza Sababu Hapa

Mkali wa Bongo Fleva Tanzania, Barnaba Elias, ‘Barnaba Classic’ ameamua kuajiri bodigadi wa kumlinda kwa ajili ya kujiongezea thamani.

Barnaba akizungumza na Showbiz alisema kuwa, ameamua kuongeza ‘value’ kwenye kazi zake na pia kuepukana na rapsha zisizo za lazima.


“Kuwa na bodigadi ni kuongeza value ya kazi yangu lakini pia kama wasanii kuna rapsha mbalimbali ambazo tunakutana nazo kutoka kwa watu ambao hawatutakii mema. Mashabiki wangu wasiniogope na kunitenga kwa sababu ya mlinzi wangu,”
alisema Barnaba.

No comments